Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Marketing Executive

Saturday, August 11, 2018

MKAA WA MATUMIZI YA NYUMBANI UNAOTENGENEZWA KWA MAKAA YA MAWE MKOA WA SONGWE


JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA RAIS
TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA


OFISI YA MKUU WA MKOA WA SONGWE





1:0 UTANGULIZI
Mkoa wa Songwe upo eneo la Nyanda za Juu Kusini Magharibi mwa Tanzania. Mkoa una kilometa za mraba 27,656 sawa na asilimia 3.1 ya eneo lote la Tanzania ukiwa na latitudo 7º na 9º 36’ kusini ya Ikweta na longitudo kati ya 32º na 33º 41’ Mashariki ya Greenwich.  Mkoa unapakana na nchi za Zambia na Malawi upande wa Kusini, Mikoa wa Rukwa  na Katavi upande wa Magharibi, Kaskazini na Mashariki Mkoa wa Tabora na  Mbeya.
Mkoa una Wilaya 4, Halmashauri 5,  Tarafa 12,  Kata 94, Vijiji 307, vitongoji 1,493, Mitaa 71, jumla ya  kaya 226,428 na jumla ya watu 1,125,520.

2. MAKAA YA MAWE
Makaa ya mawe ni aina ya mwamba mashapo au mwamba metamofia na fueli kisukuu muhimu. Mwamba ulitokea kutokana na mabaki ya mimea ya kale yaliyogeuzwa kuwa aina ya mwamba katika mchakato wa miaka mamilioni. Kikemia  makaa ya mawe ni kaboni.
Asili ya makaa ya mawe ni mabaki ya mimea iliyokufa miaka mingi iliyopita. Mabaki ya mimea yanapofunikwa kwa maji au kuzama katika matope hayaozi  kama jinsi ilivyo kutokea kwa mboji. Kinachotokea ni ganda la nyuzi za mimea zinazokauka wakati maji yanapopungua. Maganda haya ni kitangulizi cha makaa ya mawe. Ubora wa kiuchumi na kiwango cha nishati kilichomo katika makaa unaongezeka kadri ya umri wake na kina cha mahali panapochimbwa
Mkoa wa Songwe una  makaa wa mawe katika wilaya ya Mbozi, Ileje na Songwe ambayo ni Magamba, Kiwira na Kabul.



3. UTENGENEZAJI WA  MKAA
Teknolojia ya  utengenezaji wa mkaa bora wa kupikia ni teknolojia inayopatikana wilaya ya Mbozi Mkoani Songwe katika machimbo ya Makaa ya Mawe ya Magamba.  Utafiti ulifanyika mwaka 2017 na Mchumi Mkuu wa Mkoa wa Songwe kwa kushirikiana  na Kitengo cha ubora wa Makaa ya mawe kutoka Tancoal Energy Limited kilichopo mgodi wa Ngaka wilayani Mbinga Mkoa wa Ruvuma.
Matokeo ya teknolojia hii yanatoa jibu  la matatizo yaliyodumu kwa  muda mrefu yaliyotokana na ukataji miti kiholela kwa ajili ya matumizi ya nishati.Teknolojia ya Makaa bora ya  briketi ni rahisi, na ni mbadala wa nishati, ni suluhisho kwa kero za kuni na mkaa kwa matatizo 

mateso yatokanayo na nishati hizo zitumikazo kwa matumizi ya nyumbani na katika taasisi mbalimbali.
Mkaa unatengenezwa kwa mchanganyiko wa chenga chenga ( vumbi) la makaa ya mawe , udongo  mfinyanzi, virutubisho, mabaki ya mazao ya kilimo yaliyokauka na maji katika vipimo maalumu.

Briketi za makaa ya mawe zaweza kutengenezwa kwa mikono kwa kutumia kifaa kilichotengenezwa maalum kwa bati gumu (hand molder).



3.2  MUDA WA KUKAUKA
Briketi za makaa bora huchukua muda wa siku 2 au 3 kukauka kulingana na hali ya hewa baada ya kutengenezwa.

3.3 KIPINDI CHA MASIKA/ MVUA
Kipindi cha masika ni rahisi njia mbadala ya kukausha nishati hii huweza kukaushwa katika tanuru, au kivulini baada ya kutengenezwa.





No comments:

Post a Comment