Katika
kufanikisha uhifadhi na utunzaji wa mazingira serikali ya Jamhuri ya Tanzania
imefanikisha kuwepo kwa maonyesho ya matumizi ya nishati mbadala katika suala
zima la matumizi ya mkaa unaotokana na taka,masalia ya viumbe hai(makaa ya
mawe),na mabaki ya mbao.
Katika kufanikisha hilo Wizara ya Mazingira Nyumba na
Makazi chini ya Mh January Makamba
imetoa fursa kwa Taasisi,Asasi,za kiserikali na zisizo za serikali(binafsi)
kuonyesha uwezo wa kuhakikisha miti inabaki salama kwa kuzalisha mkaa mbadala.
Maonyesho haya yanafanyika katika viwanja vya
maonyesho MNAZI MMOJA jijini
Dar Es Salaam kwa muda wa siku
5.Maonyesho haya yamefunguliwa na Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania
Mh Majaliwa Kasim Majaliwa.
Katika maonyesho haya kuna mabanda zaidi ya 20
yanayotoa elimu ya matumizi ya nishati mbadala na utunzaji wa
mazingira,kuendana na kauli mbiu ya mwaka NITUNZE
NIKUTUNZE.
Baadhi ya wadau wanaoshiriki katika maonyesho haya ni AG
ENERGIES, GREEN POWER GROUP,KIPEPEO RECYCLERS,ENVOTEC SERVICE LTD,ZAID
RECYCLERS,BSM,MENA WOOD BRIQUETING CO.LTD,LISTAF ENTERPRISE SOLITION,MABAKI
MALI,MKAA POA HALISI,MCHAU WINDMILL ENTERPRISES,DEMACO MOROGORO,WASTEWATER
SOLUTIONS,EDO SAMA,TANZANIA BIOMIC CO.LTD,ALPECH,SIMUSOLAR,SIX STAR HOLDING
LTD,ZOLA,OFISI YA MKUU WA MKOA WA SONGWE,TATC,TANPACK TISSUES LTD,GOODFIRE
BRIQETTES,JIKO MATAWI,JHS,SUNKING,SIGA ENTERPRISES,FAMILY HERBAL
CLINIC,TANZANIA AIRPORT AUTHORITY(TAA),WIZARA YA MALIASILI NA UTALII,MKAA
ENDELEVU,MKAA MKOMBOZI,SNV,BORDA, na IDARA YA MAMLAKA YA HALI YA HEWA.
guta86.blogspot.com
imefanikwa kutembelea maonyesho haya na kufanya mzungumzo na baadhi ya viongozi
na wafanyakazi wa wadau hao.Edwin86
aliongea na Mr James,Jesca Elias na Gemma Kavishe wa Six Star Holding Ltd,Irene
Missanga Muja(CEO) wa Mabaki Mali,Leah Nyengo wa Mena Wood Briqueting Co.Ltd,Mr
Godlove Ngoda wa BORDA,na
wengine wengi.Pia Edwin86 amekutana na
kufanya mazungumzo na Mh John
Hagu Mratibu Mkuu wa UWAMITA (Mifuko
mbadala Tanzania)
Kilele cha maonyesho haya ni tarehe 5//2018 hapa hapa
Mnazi Mmoja Jijini Dar Es Salaam.
Imeandaliwa
na Kulipotiwa na Edwin86 wa guta86.blogspot.com.
No comments:
Post a Comment