ODM Film Company kampuni bora kabisa kwa uandaaji na utayarishaji wa video za aina tofauti ama mbalimbali imekamilisha kipindi cha TV kinachojulikana kwa jina la FURSA chenye kauli mbiu isemayo NAFASI NI YAKO.Kipindi hiki chenye ubora wa hali ya juu na kinachoelimisha jamii kimeandaliwa chini ya Madirector wawili wenye uzoefu mkubwa wa kuandaa vipindi vya aina hii ambao ni Ali .B.Osenga na Damu Niwagira.
Kipindi hiki kimebuniwa na kuhaririwa na Edwin Malima ambae pia ni Mtangazaji wa kipindi hiki akishirikiana na Amboni Patrick ambae ni mtangazaji wa kike.
Unaweza tembelea pia Youtube chanel ya ODM TZ ama instagram page odmfilm kwa taarifa zaidi.
No comments:
Post a Comment