Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Marketing Executive

Monday, April 23, 2018

MASOGANGE WA BELLE 9 AFARIKI


Video queen maarufu Bongo Agness Gerald maarufu kama Agness Masogange amefariki Dunia leo katika Hospitali ya Mama Ngoma iliyoko Mwenge, Wilaya ya Kinondoni, jijini Dar es Salaam.

Alikuwa anasumbuliwa na Homa ya matumbo pamoja na tatizo la kupungukiwa na damu.
Akithibitisha taarifa ya kifo hicho Daktari Rama Ngoma wa hospitali ya Mama Ngoma, amesema Agnes amefariki dunia kwa tatizo la pneumonia na upungufu wa damu jioni hii, na alikuwa amelazwa hospitalini hapo kwa muda wa siku nne mpaka kifo kilipomkuta.


Tayari mwili wake umeshatolewa hospitali ya Mama Ngoma, na kwa mujibu wa muigizaji Steve Nyerere umepelekwa hospitali ya Taifa ya muhimbili.

Mungu ailaze roho yake mahala pema peponi.




No comments:

Post a Comment