Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Marketing Executive

Wednesday, September 12, 2018

MKAA SONGWE WAHITAJI UWEKEZAJI

Uongozi wa Mkoa mpya wa Songwe chini ya Investment Coordinator wa Mkoa huo Bi Halima Mpita unaoendelea na uzalishaji wa mkaa wa matumizi ya nyumbani unaotokana na makaa ya mawe unaelekeza nguvu katika eneo zima la uwekezaji.Uongozi unajaribu kuendelea kutoa rai kwa Watanzania wote wenye uwezo wa kushirikiana na Serikali katika kuwekeza katika miradi mikubwa na midogo inayoanzishwa ndani ya nchi.

Rai hiyo imetolewa baada ya mradi huu kufika katika hatua nzuri na stahiki kuruhusu wawekezaji wa ndani na nje kuanza kuwekeza ili kupanua wigo wa mradi huu lengo ikiwa ni kuongeza ajira,kukuza uchumi na kuhifadhi mazigira.

Wawekezaji ama wadau wa sekta ya biashara na viwanda wanakaribishwa kuja kuwekeza katika mradi wenye faida kubwa kiuchumi.Mradi huu wa uzalishaji wa mkaa wa majumbani maarufu kwa jina la Mkaa Songwe unaotokana na makaa ya mawe ni jibu tosha la utunzaji wa mazingira hasa katika ukataji miti.Pia huendana na kipato cha Watanzania walio wengi kwani hupatikana kwa gharama nafuu sana.

Wadau ama wawekezaji wanaweza kuwekeza katika suala zima la vifungashi(packaging),Matangazo,Uingizaji wa Mkaa Songwe nchi nzima sokoni(Marketing) na uwekezaji katika eneo zima la uongezaji wa mashine za kisasa zaidi ili kukidhi mahitaji ya wateja.

kwa mawasiliano piga smu namba +255 719 797 295 or email address 86guta@gmail.com.

No comments:

Post a Comment