Ali Kiba maarufu kama King Kiba amekua msanii maarufu nchini Tanzania kuweza kudumu katika mahusiano yasiyokua na skendo hadi kufikia kufunga ndoa halali kwa mujibu na taratibu za kidini.
Ali Kiba akiambatana na rafiki yake wa karibu Ommy Dimpoz walifika mbele ya Rais Mstaafu Mh Jakaya Kikwete na kupokea baraka juu ya ndoa yake hiyo.
Ali Kiba ameweza kuonyesha jamii nzima hasa Afrika Mashariki kua anajitambua na anafuata taratibu zote halali katika suala hilo.
No comments:
Post a Comment