BUNGENI:
Spika Job Ndugai amesema ameagiza Wabunge wasiingie na 'power bank' wala chaja
za simu ndani ya ukumbi wa Bunge.
Hii
ni kutokana na mlipuko uliotokea wakati wa kikao cha Bunge baada ya 'power
bank' ya Mbunge wa Nsimbo, Richard Mbogo kupata hitilafu hali iliyopelekea
kikao hicho cha Bunge kuahirishwa
Aidha
Wabunge wamesisitiza Katibu wa Bunge afikirie kumpongeza Askari aliyejitoa
mhanga na kuitoa nje 'power bank' iliyokuwa ikiwaka moto kwani alionesha
ujasiri mkubwa .
No comments:
Post a Comment