Mama Mzazi wa msanii maarufu wa kike
nchini Tanzania Lady Jay Dee amefariki na kuwapa wakati mgumu familia yake na
wakazi wa eneo hilo.
Mzazi huyo ametoweka ama amekumbwa na
mauti baada ya kuugua kwa muda mrefu na jana siku ya Alhamis ndipo mauti
ilipomkuta.
Msiba huo unawalenga watanzania wote
na hasa wakazi wa Kiwalani alipokua akiishi mama Jide.
Guta86.blogspot.com kupitia kwa
mwakilishi wake anaejulikana zaidi kwa jina la Rymes ilipata taarifa hizo kwa
njia ya simu kutoka kwa mdogo wa Jide anaekwenda kwa jina la Dabo.
Kutokana na taariffa hizo
Guta86.blogspot.com inawapa pole wafiwa wote na Watanzania kwa ujumla.
Mungu ailaze mahala pema peponi roho ya Maerehem.
No comments:
Post a Comment