Drop Down MenusCSS Drop Down MenuPure CSS Dropdown Menu

Marketing Executive

Saturday, August 11, 2018

MKAA WA MATUMIZI YA NYUMBANI UNAOTENGENEZWA KWA MAKAA YA MAWE MKOA WA SONGWE.


Makaa ya mawe ni aina ya mwamba mashapo au mwamba metamofia na fueli kisukuu muhimu kwa lugha ya kitaalamu kwa Kiswahili.

Ubora wa kiuchumi na kiwango cha nishati kilichomo katika makaa unaongezeka kadri ya umri wake na kina cha mahali panapo
chimbwa.
Mkoa wa Songwe umekua maarufu kwa utoaji wa makaa ya mawe hasa katika wilaya ya Mbozi,Ileje na Songwe ambayo ni Magamba,Kiwira na Kabul .
                       Bi Halima Mpita akiwa katika uzalishaji TIRDO jijini Dar es Salaam

Utengenezaji wa mkaa kwa matumizi bora ya kupikia majumbani maarufu kama mkaa songwe ni teknolojia inayopatikana wilaya ya Mbozi mkoani songwe katika machimbo ya makaa ya mawe ya MAGAMBA,na utafiti ulifanyika mwaka 2017chini ya mtaalamu wetu na Mchumi mkuu wa Mkoa wa songwe Bi Halima Mpita kwa kushirikiana na kitengo cha ubora wa makaa ya mawe kutoka Tancoal Energy Limited kilichopo wilaya ya Mbinga mgodi wa Ngaka.
                                          Bi Halima Mpita akiwa katika mgodi wa Ngaka

Teknolojia hii ni suluhisho kwa kero za kuni na mkaa inayopelekea ukataji wa miti na kuharibu mazingira kwa ujumla jambo linalochangia kuongeza hali ya ujangwa nchini,mvua zinazoambatana na madhara,mabadiliko ya hali ya hewa,uharibifu wa makazi ya viumbe hai wa porini,kuharibu vyanzo vya maji,na kuondoa uoto wa asili ,nk.





Mkaa Songwe unaotokana na makaa ya mawe umetengenezwa kwa mchanganyiko wa chenga chenga[vumbi]la makaa ya mawe ,udongo mfinyanzi,virutubisho,mabaki ya mazao ya kilimo yaliyokauka,na kuchanganywa na maji katika kiwango maalumu.

KIPINDI CHA MVUA
Mkaa songwe umekua suluhisho kwa wakazi wa mkoa wa songwe kwani ni rahisi kukausha nishati hii kwa kutumia tanuru au kivulini baada ya kutengenezwa na kutumika kwa kupikia.



UWAKAJI
Mkaa songwe mkaa bora wa mgodi wa Magamba huwaka vizuri ,moto unapoanza kuwaka hutoa ulimi mfupi rangi ya bluu kutoka katika jiko la kawaida ,mkaa songwe ukishawaka hautoi moshi wala kutengeneza masizi ambayo yanachafua sufuria na vipande vidogo 34 vya mkaa huifadhi moto kwa saa 3 hadi 4 bila kuzima.
Mkaa songwe ni mkaa bora na safi kwa matumizi ya kupikia unaowashwa kwaurahisi sana kama mkaa wa kawaida.


No comments:

Post a Comment